Dobrindt apuuza mvutano katika uteuzi wa majaji wapya
12 Julai 2025Matangazo
Siku ya Jumamosi, Dobrindt ameliambia shirika la habari la Deutschlandfunk kwamba hawezi kukubaliana na hoja iliyotolewa na wakosoaji kwamba chochote ambacho hakitoi matokeo ya aina fulani ya moja kwa moja, kinaleta madhara ya moja kwa moja kwa Mahakama ya Kikatiba.
Kiongozi wa chama cha upinzani cha KijaniFranziska Brantner, aliwaambia waandishi wa habari kwamba imani katika mahakama hiyo ya juu zaidi imeharibiwa kiholela.
Mzozo kati ya makundi mawili katika serikali ya muungano, ambayo ni chama cha kihafidhina na cha Social Democratic (SPD) ulisababisha kucheleweshwa kwa kura ya kuwachagua majaji hao wapya wiki hii.