MigogoroUrusi
Dmitry Medvedev: Urusi inasaka ushindi tu, si makubaliano
3 Juni 2025Matangazo
Ameandika kwenye mtandao wa Telegram kwamba mazungumzo yaliyofanyika Istanbul hayakulenga kuleta maelewano ya amani kwa masharti ya kumlaghai mwingine ila yalilenga kuwahakikishia ushindi na kuuangusha kabisa utawala wa kinazi.
Amesema hayo wakati ujumbe wa maafisa wakuu wa Ukraine ukitua Washington hii leo kwa mazungumzo na maafisa wa Marekani kuhusu masuala ya ulinzi na uchumi.
Msaidizi wa Rais Volodymyr Zelensky, Andriy Yermak, amesema wamekwenda kuzungumzia msaada wa ulinzi na hali katika uwanja wa vita, kuimarisha vikwazo dhidi ya Urusi.