Dereva auvamia umati na kuua mmoja, Mannheim- Ujerumani
3 Machi 2025Matangazo
Polisi imesema imemkamata mtuhumiwa wa tukio hilo na imewatolea mwito wakaazi wa mji huo kubakia majumbani na kutokaribia eneo la katikati mwa mji.
Msemaji wa polisi amearifu kwamba dereva aliendesha gari kwa kasi na kuliparamia kundi la watu kwenye mtaa wenye shughuli nyingi wa mji huo.
Polisi imesema imeanzisha uchunguzi kubaini sababu za mkasa huo na bado haina maelezo ya kutosha juu ya iwapo kisa hicho kilipangwa kwa kuhusisha watu wengine.