UchumiChina
China: "Tunatafakari ombi la Marekani kuzungumzia ushuru"
2 Mei 2025Matangazo
China aidha imeitaka Marekani kuwa tayari kufuta ushuru uliozorotesha masoko ya kimataifa na minyororo ya ugavi.
Wizara ya biashara ya Beijing imethibitisha kuwa Marekani ilifanya mawasiliano na kwamba "kwa sasa wanatathmini" pendekezo hilo.
Amesema ikiwa Marekani inataka kuzungumza, inapaswa kuonyesha uaminifu, kuwa tayari kurekebisha mazoea mabaya na kufuta ushuru wake wa upande mmoja.
Marekani iliiadhibu China kwa ushuru wa hadi asilimia 145 kweyne bidhaa nyingi za China ulioanza kutumika mwezi Aprili na Beijing ikajibu kwa kutoza ushuru mpya wa asilimia 125 kwa bidhaa zinazoagizwa kutoka Marekani.