Uchumi
China yaapa kujibu hatua ya Marekani ya kuiongezea ushuru
28 Februari 2025Matangazo
Wizara ya biashara ya China pia imeonya kwamba hatua hiyo iliyochukuliwa na Marekani, haitokuwa na mchango mzuri katika kutatuwa matatizo yake, isipokuwa itayaongezea mzigo makampuni ya Marekani na wateja wao, pamoja na kuhujumu uthabiti wa viwanda duniani.
Mpango huo wa Marekani uliotangazwa hivi karibuni dhidi ya China, Canada na Mexico utaanza kutekelezwa Jumanne ijayo na umeongeza makali ya vita vya kibiashara kati ya China na Marekani, mataifa mawili makubwa kiuchumi duniani.