SiasaChina
China na Urusi kufanya luteka ya pamoja ya kijeshi
30 Julai 2025Matangazo
Msemaji wa wizara ya ulinzi wa China, Zhang Xiaogang amesema luteka hiyo ya pamoja ya kijeshi ni sehemu ya mipango ya mara kwa mara ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili na wala haimlengi yeyote, akisisitiza kuwa baadaye China na Urusi zitafanya doria kwenye Bahari ya Pasifiki.
Kando na uhusiano wa kiuchumi na kisiasa, Urusi na China zimeimarisha pia ushirikiano wa kijeshi katika miaka ya hivi karibuni, huku nchi hizo mbili zikijaribu kukabiliana na kile wanachokitaja kuwa utaratibu wa kimataifa unaoongozwa na Marekani.