China na Marekani zalegeza masharti ya kibiashara
27 Juni 2025Matangazo
Marekani nayo ikiondoa hatua kali za kibiashara ilizoiwekea China.
Awali Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kutiwa saini mkataba wa kibiashara kati ya nchi yake na China na kugusia kwamba unajumuisha usafirishaji wa smaku na madini adimu kutoka Beijing kwenda Washington.
China na Marekani kujadili mvutano wa kibiashara
Tangu Trump aanzishe vita vya biashara na China mwezi Februrari, mataifa hayo mawili yenye uchumi mkubwa zaidi duniani yamekuwa katika mvutano wa kupandishiana ushuru ambao umevuruga masoko ya dunia.
Kwengineko Trump pia amedokeza kuwa huenda kukawa pia na makubaliano makubwa ya kibiashara kati ya taifa hilo na India.