Uchumi
China, Marekani zaendelea na mazungumzo ya kibiashara Geneva
11 Mei 2025Matangazo
Katika mazungumzo hayo ya faragha, Marekani inawakilishwa na Waziri wa fedha Scott Bessent na kwa upande wa China anayeiwakilisha ni Naibu Waziri Mkuu He Lifeng.
Soma zaidi: Wawakilishi wa China na Marekani wakutana kujadili namna ya kutuliza mvutano wa kibiashara
Majadiliano kati ya nchi hizo yalianza Jumamosi. Yanafanyika katikati ya vita vya kibiashara viliyochochewa na hatua ya mwezi uliopita ya Rais wa Marekani Donald Trump kuyawekea ushuru mkubwa mataifa kadhaa ulimwenguni na hivyo kuvuruga minyororo ya ugavi, ustawi wa masoko na kuzusha hofu ya kuzorota kwa ukuaji wa uchumi kote duniani.