SiasaVenezuela
Chama cha Maduro kushinda ubunge, ugavana Venezuela
26 Mei 2025Matangazo
Muungano wa upinzani unaoongozwa na Maria Corina Machado ulikuwa umewataka wapigakura kujitenga na uchaguzi huo, kupinga uchaguzi wa mwaka jana uliomrejesha madarakani Rais Nicolas Maduro.
Soma zaidi: Venezuela yawaachia Wamarekani sita baada ya kukutana na mjumbe wa Trump
Shirika la habari la AFP limeripoti idadi ndogo kabisa ya wapigakura vituoni, huku zaidi ya maafisa 400,000 wa usalama wakitumwa mitaani, ambapo zaidi ya watu 70 walikamatwa kuelekea uchaguzi huo.
Shirika linalofuatia maoni ya wapigakura la Delphos linasema waliojitokeza kupiga kura kuwachaguwa wabunge 285 na magavana 24 ni asilimia 16 tu ya wapigakura halali.