Chama cha Machar chatangaza kuvunjika mkataba wa amani
27 Machi 2025Kiongozi huyo amesema hatua hiyo sasa inatishia kuitumbukiza tena nchi hiyo katika vita.
Marekani leo imetoa wito kwa Rais Salva Kiir kumwachilia huru mpinzani wake Riek Machar anayedaiwa kuwa chini ya kifungo cha nyumbani, na kusema sasa ni wakati kwa viongozi hao kuonyesha kujitolea kwao kwa amani.
Katika chapisho kwenye mtandao wa X, ofisi ya Marekani ya masuala ya Afrika, imesema wana wasiwasi kutokana na ripoti kwamba Machar yuko chini ya kifungo cha nyumbani.
Ofisi hiyo imemuhimiza Rais Kiir kubatilisha hatua hiyo na kuzuia kufanya hali hiyo kuwa mbaya zaidi.
Hata hivyo jeshi la serikali ya nchi hiyo pamoja na msemaji wa serikali hawakujibu mara moja ombi la tamko kuhusu hali hiyo.
Hapo jana chama cha Machar cha SPLM-IO, kilisema kuwa waziri wa ulinzi na mkuu wa usalama wa kitaifa waliingia kwa nguvu katika makazi ya Machar na kuwasilisha waranti ya kukamatwa kwake.